Tuesday, August 7, 2012

DIRA YA MABADILIKO – VISION FOR CHANGE: MANIFESTO YA CUF YA 2010


A Vision for Change
“Watanzania wameweka matumaini yao kwa Chama cha CUF na misingi yake ya sera ya kuleta “Haki sawa kwa wananchi wote” na “Kujenga uchumi imara unaoongeza ajira na utakaoleta neema na tija kwa wote.” Chama chetu kimekuwa ni Chama kikuu cha upinzani nchini kwa muda mrefu sasa na wananchi wanaendelea kuteseka kwa kuona matatizo yao yakizidi kuongezeka bila kuchukuliwa kwa hatua za msingi kushughulikia matatizo yao. Hali hii inawafanya wananchi wengi hasa vijana na wanawake kuwa katika shauku kubwa ya kuona utawala wa nchi yetu unabadilishwa kwa amani kupitia karatasi za kura. CUF kwa kutambua nafasi yake katika kuyaongoza Mabadiliko yanayohitajika, kikiwa siyo tu chama kikuu cha upinzani hapa nchini bali pia kutokana na mjengeko wake wa kuwa kweli ni chama cha kitaifa chenye kukubalika na chenye mtandao mpana katika pande zote mbili za Jamhuri ya Muungano, imezindua DIRA YA MABADILIKO – VISION FOR CHANGE. Dira ya Mabadiliko ndiyo msingi wa ILANI yetu ya uchaguzi. Vision for Change chini ya Serikali ya CUF itatujengea Tanzania Mpya inayojali haki sawa kwa wananchi wote na itakayojenga uchumi imara unaoongeza ajira na utakaoleta neema na tija kwa wote.” Kwa kuisoma Manifesto yetu ya Uchaguzi Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wa mwaka 2010, unaweza kupakuwa kwenye kiungo hapo chini.
 CUF Manifesto 2010

No comments:

Post a Comment