Saturday, August 25, 2012

MUDA WA KULITEKA JANGWA UMEWADIA.

Mh Abdul Kambaya-
Naibu Mkurugenzi wa Habari,
Mahusiano na Haki za Binadamu
wa Chama cha Wananchi (CUF)
KATIKA KUJIANDAA NA SAFARI YA KUELEKEA ARUSHA TUTALIKABILI JANGWA TAREHE 09-09-2012
CUF-Chama Cha Wananchi, kinawatangazia Mkutano Mkubwa wa Hadhara utaofanyika siku ya Jumapili kwa tarehe tajwa hapo juu.
Mkutano huo unatarajiwa kuhudhuriwa na Viongozi wote wa Kitaifa wa CUF. Mkutano utaanza saa nne asubuhi mpaka saa kumi na mbili jioni. Profesa Ibrahim Lipumba atawaoongoza Wanachama wa CUF katik

a Mkakati mdogo Ujulikanao kwa jina la MCHAKA MCHAKA MPAKA 2015 kuzunguka Mikoa sita kukutana na Watanzania ili kuweza kujadili muelekeo wa Nchi yetu na hatima ya Watanzania chini ya siasa Uchwara za Serikali ya Chama cha Mapinduzi. Kila Mwanacuf unaesoma taarif a hii, tafadhali mjulishe na mwenzio. Makabwela na Walala hoi wote tafadhalini ASIBAKI MTU NYUMBANI . Mabepari wamefanya Mkutano wao na mmewashuhudia, sasa ni zamu ya MAKABWELA NA WALALA HOI kukumbuka historia ya mababu zetu ndani ya Jangwa la MAKABWELA. MCHAKA MCHAKA MPAKA 2015

No comments:

Post a Comment