Wednesday, December 26, 2012

UCHUMI WA DUNIA UNAELEKEA WAPI IFIKAPO 2030?

Mwenyekiti Wa CUF-Prof Ibrahim H Lipumba

Tangu mwaka 1997, Baraza la Kijasusi la Taifa la Marekani (The National Intelligence Council (NIC)) linatoa taarifa kuhusu mielekeo muhimu ya Dunia (Global Trends) kila baada ya miaka minne kufuati kumalizika kwa uchaguzi wa Rais wa Marekani. Mwezi huu wa Desemba Baraza hilo limetoa taarifa yake ya tano ya Mielekeo ya Dunia 2030 (Global Trends 2030). Taarifa hii inachambua muelekeo wa kiuchumi, kisiasa, kijamii na kiusalama kwa miaka 15 ijayo mpaka ifikapo 2030. Madhumuni ya taarifa hii ni kusaidia viongozi na hususan Rais wa Marekani kuelewa mielekeo muhimu ya dunia ambayo inastahiki kuzingatiwa katika kubuni na kutekeleza sera zenye lengo ya kulinda maslahi ya Marekani.
Global Trends 2030 inaonyesha kuwa katika nyanja za uchumi, China itaongoza na kuwa na uchumi mkubwa kuliko Marekani miaka michache kabla ya 2030.Mchango wa nchi za Ulaya Magharibi, Japan na Urusi katika uchumi wa dunia utaendelea kupungua. Nchi za Asia na hasa China na India zitakuwa na nguvu kubwa za kiuchumi na kijeshi. Ukiritimba wa Marekani wa nguvu za kiuchumi, kisiasa na kijeshi ulioanza baada ya vita vya pili mwaka 1945, hivi sasa unaporomoka kwa kasi kubwa.
Kwa kutumia kipimo kinachojumuisha ukubwa wa uchumi, wingi wa watu, uwekezaji katika teknolojia na matumizi katika majeshi na vyombo vya ulinzi, China itakuwa na nguvu na uwezo zaidi kuliko Marekani. Hata hivyo Marekani itaendelea kuwa na nguvu nyepesi (soft power) kwa kuendelea  kuwa na mvuto mkubwa zaidi katika medani ya utamaduni kama vile muziki, sinema, vyombo vya habari, michezo ya riadha, na uwezo wa kushirikiana na nchi nyingine hasa zile zenye mifumo ya kidemokrasia.
Mielekeo mikubwa iliyochambuliwa na Global Trends 2030 ni ongezeko kubwa la uwezo wa watu binafsi kwa sababu ya kuongezeka kwa kipato na kupungua kwa umaskini. Watu wanaoishi katika tabaka  la kati (middle class) katika nchi nyingi na hasa za Asia wataongezeka kwa kiasi kikubwa. Historia inaonyesha kuwa ongezeko la wananchi wenye kipato cha tabaka la kati huambatana na madai ya kushiriki katika maamuzi ya mambo yanayogusa maisha yao na kwa hiyo kudai na kushamiri kwa mifumo ya demokrasia.
Marekani itapoteza ukiritimba wa nguvu za kiuchumi, kisiasa na kijeshi lakini hapatatokea nchi nyingine kuwa na nguvu na uwezo kama wa Marekani katika miaka ya 1945 mpaka 2010. Mashirikiana baina ya nchi ndiko kutawezesha nchi hizo kuweza kuwa uwezo na ushawishi katika siasa za kimataifa.
Nchi zilizoendelea hivi sasa nchi za Ulaya na Japan pamoja na China zitakabiliwa na ongezeko la wazee na kupungua kwa vijana. Kasi ya ongezeko la watu katika nchi hizi utapungua sana na nyingine kama Urusi na Japan zitakabiliwa na kupungua kwa wingi wa watu. Uwiano wa watu wenye umri wa kufanya kazi ukilinganisha na wazee waliostaafu utapungua sana na kuweza kusababisha tatizo kubwa la kuhudumia wazee. Baadhi ya nchi hizi zitahitaji wahamiaji kutoka nchi nyingine ili kufanikisha azma ya kukuza uchumi na kuhudumia wazee waliostaafu.
Nchi nyingi za Afrika ikiwemo Tanzania zitaendelea kuwa na vijana wengi. Changamoto ya kuongeza ajira itaendelea kuwa kubwa. Nchi zitakazoweza kuongeza ajira ya vijana zitakuza uchumi wake kwa kasi kubwa. Ikiwa nchi zitashindwa kuongeza ajira, wingi wa vijana ambao hawana matumiani katika maisha yao kutachochea uvunjifu wa amani na vurugu za kisiasa.
Watu wengi watahamia mijini. Dunia kwa ujumla itakuwa na watu wengi wanaokaa mijini kuliko wanaokaa vijijini. Nchi ambazo hazina mipango miji mizuri na uwekezaji katika miundombinu zitakuwa na miji yenye maeneo mengi ya ovyo (slums) ambayo yatakuwa vituo vya makosa ya jinai na matumizi ya nguvu.
Dunia kwa ujumla itakuwa na mahitaji makubwa ya chakula, maji na nishati.Upungufu wa chakula na maji kwa matumizi ya binadamu utaathiriwa sana na mabadiliko ya tabia nchi. Ukame utaongezeka katika nchi ambazo hazipati mvua za kutosha. Mvua nyingi kupia kiasi na mafuriko yatatishia nchi ambazo zinapata mvua nyingi hivi sasa. Matukio ya hali ya hewa iliyovuka mipaka kama vile ukame wa kutisha na tufani na dhoruba zitaongezeka na kuathiri sana maisha ya binadamu na uzalishaji wa chakula.
Kuongezeka kwa watu wenye kipato cha tabaka la kati ambao watataka kuwa na gari na vifaa vya umeme kama vile friji na viyoyozi kutaongeza mahitaji na matumizi ya nishati na kuongeza hewa ukaa (greenhouse gases) inayoongeza joto duniani na kuchochea mabadiliko ya tabia nchi.
Uchumi wa dunia utakabiliwa na mahitaji makubwa ya chakula, maji, nishati na malighafi za viwanda. Suala la msingi ni vipi ushindani wa kupata bidhaa kama vile chakula, mafuta ya petroli na gesi, chuma, shaba na madini mengine kunaweza kusababisha migogoro ya kuichumi, kisiasa na kiusalama. Mtikisiko wa sekta ya fedha na uchumi uliotokea mwaka 2008 na ambao bado unaathiri uchumi wa dunia itadhibitiwa au itaendelea kutokea? Je nchi zitashirikiana ili kusimamia utandawazi uwe na manufaa kwa washiriki wote wa uchumi wa dunia na kuzuia athari kubwa zisitokee na uchumi wa dunia kuporomoka?
Je serikali na asasi za kimataifa zitakuwa na uwezo wa utawala bora wa kukabiliana na mabadiliko yatakayotokea katika uchumi wa dunia na kuweza kubuni na kutekeleza sera muafaka zinazokwenda na mabadiliko yanayotokea?
Je Marekani itaelewa na kukubali kuwa ukiritimba wa nguvu zake za kiuchumi, kisiasa na kijeshi umeporomoka na kukubali kutoa nafasi na kushirikiana na mataifa mengine na hasa China ambayo nguvu zake za kichumi na kijeshi zitaongezeka? Uongozi wa dola ya Marekani na hasa kushindwa kufikia mwafaka kati ya Bunge la Wawakilishi linaloongozwa na Republican, na Rais Obama na Baraza la Senate lenye maseneta wengi wa Chama cha Demokrati kunaashiria kuwa Marekani, inaweza kuwa na tatizo la kuwepo kwa utawala bora wenye uwezo wa kukubali na kuyashughulikia ipasavyo mabadiliko  makubwa yanayopunguza ukiriritimba wa dola ya Marekani katika mahusiano ya kimataifa.
Ukuaji wa uchumi wa dunia umechochewa na mabadiliko ya teknolojia. Katika miaka 15 ijayo mabadiliko gani ya teknolojia yanaweza yakaongeza ukuaji wa uchumi na kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi na ongezeko kubwa la watu watakaokuwa wanaishi mijini?
 Mabadiliko ya teknolojia ya kuchimba gesi na mafuta yanaweza kusababisha mabadiliko makubwa ya uchumi. Makampuni ya Marekani yamevumbua teknolojia inayoweza kuchimba gesi na mafuta yaliyoko kwenye miamba ya mawe chini ya ardhi ambayo siku za nyuma iliaminiwa kuwa gesi na mafuta hayo hayawezwi kuchimbwa. Ongezeko la uzalishaji wa gesi toka kwenye miamba umepunguza sana bei ya gesi Marekani kwa zaidi ya asilimia 70. Marekani inategemewa kuwa mzalishaji mkubwa namba moja wa mafuta ya petroli kuzidi Saudi Arabia na Urusi ifikapo mwaka 2017. Teknolojia hii itafanya Marekani kujitegemea kwa nishati na hata kuwa muuzaji wa gesi na mafuta nchi za nje. Kuna uwezekano wa bei ya mafuta na gesi katika soko la dunia kupungua sana na kuathiri nchi zinazotegemea uuzaji wa mafuta kama vile Saud Arabia na nchi nyingine za ghuba ya Uajemi
Ongezeko la uzalishaji wa gesi umeongeza ushindani wa Marekani katika viwanda vya plastiki na kemikali vinavyotumia gesi kama malighafi. Uwekezaji mkubwa wa dola bilioni 80 utafanyika katika viwanda hivi katika miaka michache ijayo. Ulaya na hasa Ujerumani yenye viwanda vikubwa vya kemikali inaanza kutaharuki kuwa kuongezeka kwa ushindani wa Marekani katika viwanda vya kemikali kwa sababu ya bei rahisi ya gesi kutaathiri viwanda vyake.
China ina miamba mingi yenye gesi lakini bado haijamudu na kumiliki teknolojia mya ya kuchimba gesi hiyo. Teknolojia hii mpya inahitaji matumizi makubwa ya maji ambayo ni haba katika nchi ya China. Isitoshe teknolojia hii inaweza kusababisha matetemeko madogo ya ardhi ambayo athari zake zinawaeza kuwa kubwa. Ikiwa teknolojia hii itaendelezwa na ikapunguza matumizi ya maji na makampuni ya China yakamudu teknolojia hii basi nchi zinauzouza mafuta ya petroli zitaathiriwa vibaya zaidi na kuporomoka kwa bei ya mafuta.
Kupungua kwa bei ya gesi nchini Marekani kunaweza kuathiri juhudi za kuwekeza na kuendeleza nishati mbadala ya jua, upepo na bayogesi na kwa hiyo kuendeleza uchafuzi wa mazingira.
Teknolojia ya viwanda pia inaendelea kubadilika. Matumizi ya kompyuta na roboti kutaka uzalishaji kunapunguza mahitaji ya nguvu kazi inayolipwa mishahara midogo. Kwa mfano utengenezaji wa bodi mama (mother board) ya Kompyuta ambacho ndiyo kifaa muhimu chenye chipu zinazoendesha na kuhifadhi nakala zote, hivi sasa kinatengenezwa na roboti badala ya binadamu. Mabadiliko haya ya teknolojia yanaweza kupunguza sana mahitaji ya wafanyakazi viwandani na yakarudisha viwanda vingi kwenye nchi zilizoendelea.
Tanzania ina wajibu wa kujipanga kutumia fursa za mieleko mikuu ya uchumi wa dunia na kujihami kwa athari zinazoweza kutokea. Kwanza kuimarisha, kuboresha na kuongeza tija katika sekta ya kilimo ni jambo muhimu kuongeza uzalishaji wa chakula kukidhi mahitaji ya ndani na kuuza katika soko la dunia. China na India zitakuwa na uchumi mkubwa na biashara ya kimataifa. Tanzania ijipange vizuri kuweza kunufaika na biashara na nchi hizo badala ya kuwa wazalishaji wa malighafi tu.
Mkakati wa kukuza uchumi unao ongeza ajira unapaswa kuzingatia mabadiliko yanayoweza kutokea. Tuandae maeneo maalum ya uchumi karibu na bandari ambayo ni makubwa yatakayosheheni miundombinu inayohitajiwa na viwanda ili gharama za uzalishaji ziwe ndogo na tuweze kuwa washindani katika soko la ndani, soko la kanda na soko la dunia.
Sekta ya gesi na mafuta iendelezwe haraka kabla ya tishio la kuporomoka kwa bei. Yajengwe mazingira ya kuanzisha viwanda vinavyotumia gesi kama malighafi. Mji wa Mtwara wenye bandari asilia uendelezwe kuwa makao Makuu ya sekta na viwanda vya gesi
Jiji la  Dar es Salaam limekua bila kufuata taratibu za mpango mji. Ni vyema tuwe na mipango mizuri ya kukuza miji yetu ili iwe na huduma na gharama nafuu za uzalishaji wa bidhaa na huduma.
Global Trends pia imechambua nchi ambazo zinaweza kuwa na misukosuko mikubwa ya kisiasa na kijamii inayoweza kusababisha kuporomoka kabisa kwa utawala wa dola (state failure) kati ya sasa na mwaka 2030. Nchi nyingi za jirani ikiwemo Burundi, Rwanda, Uganda, Malawi na Congo zinaweza kuathirika na kuporomoka kwa utawala wa dola. Tanzania inapaswa kuzingatia uwezekano huo katika kuandaa vyombo vyake vya ulinzi.
Navishauri vyombo vyetu vya ulinzi na Tume ya Mipango vipitie taarifa hii na vijipange kufanya uchambuzi wa nchi za kanda yetu ili tuweze kubuni na kutekeleza sera muafaka za kukuza uchumi unaoleta neema kwa Watanzania wote huku tukilinda mazingira na kujihami kiusalama.

Sunday, November 25, 2012

MSIMAMO WA JUMUIYA YA VIJANA KWA TFDA NA WAUZAJI WA MADAWA YA KULEVYA NCHINI.

Naibu katibu Mkuu JUVICF-Thomas Malima

 TFDA ibomolewe, isukwe upya, wahujumu wa madawa ya umma washitakiwe.
Vinara wa Madawa ya kulevya nao watajwe na kufikishwa mahakamani.
Serikali ya Tanzania kupitia wizara ya Afya, Mamlaka ya Chakula na Dawa, pamoja na Mamlaka ya Bandari vimekuwa mawakala wakubwa wa biashara haramu ya afya za watanzania. Afya za watanzania zinaendelea kuwekwa rehani na waliopewa mamlaka ya kuongoza.
Wizara ya Afya imekuwa ikiruhusu uwepo wa zahanati na maduka ya madawa yasiyo na wataalamu wa afya ambapo watanzania wengi wamekuwa wakipewa dawa zisiendana na magonjwa wanayoumwa. Hali imesababisha madhara makubwa kwa wagonjwa. Utafiti uliofanywa na Youth Initiative Tanzania (yiTa) na TWAWEZA kuanzia Novemba 2011 hadi Agosti 2012 ulibaini kuwa zaidi ya 93% ya huduma zinazotolewa katika zahanati na maduka binafsi ya dawa jijini Dar es salaam, hutolewa bila kutumia utaalamu wa afya. Je, wizara ya Afya ina mpango gani wa kukomesha hali hii?.
Pamoja na hali kuwa mbaya kiasi hicho, TFDA imekuwa ikpata kashfa kubwa za kuhatariasha maisha ya watu kila kukicha lakini hakuna hatua zozote zinazochukuliwa dhidi ya mabosi wa TFDA. Watanzania watakumbuka kuwa mwishoni mwa mwaka 2011 watafiti wa ugonjwa wa Maralia toka Uingereza wakiongozwa na Dr. Washington walitoa ripoti juu namna ambavyo Serikali za Afrika zimekuwa zikipokea madawa bandia toka China na namna ambavyo madawa hayo yanavyoathiri afya za watu. Lakin cha ajabu TFDA ilikana kupokea madawa bandia, lakini baada ya miezi miwili madawa bandia ya Maralia yakakamatwa Mwanza na Kilimanjaro. Ndipo baadaye viongozi wa TFDA walipojitokeza kwa aibu na kukiri kuwapo kwa madawa hayo bandia nchini. Lakini hakuna hatua zozote zilizochukuliwa dhidi yao.
Hivi karibuni, kumepatika dawa feki za kuongeza nguvu za waathirika wa VVU, lakini pia hakuna hatua zozote zilizokwisha chukuliwa.
Na cha kusikitisha zaidi, ni pale Watanzania wanaambiwa kuwa hakuna dawa katika hospitali za umma wakati hospitali za binafsi zina shehena ya dawa zilizoandikwa “NOT FOR SALE”. Na cha ajabu zaidi TFDA wanakili kuwa wameibiwa dawa zilizotakiwa zitolewe bure kwenye zahanati na hospitali za serikali lakini zimepotea na zinapatikana katika hospitali na maduka binafsi ya dawa zikiwa zimefutwa nembo ya NOT FOR SALE. Wakati haya yanatendeka, hospitali za umma ziko taabani, hakuna dawa. Imebaki kwenda hospitali na kupima, kisha unaambiwa nenda ukanunue dawa katika dawa Fulani. Lakini serikali imekaa kimya dhiti ya mamlaka hizi.
Jumuiya ya Vijana ya CUF (JUVICUF), inatambua kuwa endapo hatua za haraka hazitachukuliwa, kunahatri kubwa ya kuwapoteza watoto wengi ambao ndio vijana wa kesho. Akina mama na Vijana nao wako hatarini kupotea. Hivyo tunaitaka serikali kuwaachisha kazi wakurugenzi wote wa TFDA ili hatua za kisheria zichukue mkondo wake.
Nalo suala la watuhumiwa wa madawa ya kulevya limewekwa kwapuni kwa sasa. Serikali ilishahidi kutoa orodha yao lakini haitaki kutoa hadi sasa. Hili ni suala linaloathiri maisha na nguvu kazi ya vijana moja kwa moja. Vijana wengi wanapotea kwa kuathirika na madawa ya kulevya.
JUVICUF inaitaka serikali iwataje wauzaji na wasambazaji wa madawa ya kulevya nchini bila kujali vyeo na haiba yao katika jamii. Na baada ya kuwataja, wafikishwe mahakamani ili sheria ichukue mkondo wake.
Endapo serikali haitachukua hatua za kuisafisha TFDA na kuwataja pamoja na kuwafikisha mahakamani watuhumiwa wa madawa ya kulevya kama ilivyoahidi, na kwa kuwa waathirika wakubwa madawa ya Kulevya na madhara ya kuuzwa kwa dawa kiholela pamoja hospitali za umma kukosa dawa ni Vijana, JUVICUF itafanya maandamano ya amani hadi wizara ya afya kushinikiza hatua za uwajibikaji na kisheria zichukuliwe.
Imeandaliwa na:
Thomas D.C Malima
Naibu Katibu
Jumuiya ya Vijana ya CUF (JUVICUF)-Taifa.

Tuesday, November 6, 2012

MWANDISHI HUYU HANA AKILI TIMAMU?

SOMA MAKALA YAKE YENYE KICHWA CHA HABARI
PROFESSA LIPUMBA NI MBUMBUMBU WA SHERIA,ACHA SHERIA ICHUKUE MKONDO WAKE
NA HAPPINESS KATABAZI
KWA mara ya pili sasa Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF), Professa Ibrahim Lipumba  amekuwa akiitisha mikutano na waandishi wa habari kuzungumzia vurugu za kidini zilizotokea hapa nchini hususani jijini Dar es Salaam.
Profesa Lipumba pamoja na mambo mengine amekuwa akisema tena kwa ujasiri kuwa kesi ya jinai namba 245/2012 inayomkabili Sheikh Issa Ponda na wenzake 49 iliyofunguliwa na upande wa jamhuri Oktoba 18 mwaka huu, ambayo ipo mbele ya Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam, Victoria Nongwa na inendwa na wakili mwandamizi wa serikali Tumaini Kweka wakati upande wa utetezi unatetewa na wakili wa kujitegemea Mansoor Nassor ilipaswa iwe ya madai na siyo jinai na kwamba eti Ponda alistahili dhamana na kuwa anafanya mpango wa kukutana na Rais Jakaya Kikwete amshauri serikali ifanye mazungumzo na Maimamu wa misikiti ili waweze kupata suluhu ya tatizo la vurugu hizo za kidini.
Binafsi ni mwandishi wa habari za mahakamani hapa nchini na kesi hii ni miongoni mwa kesi ambazo minaziudhulia siku ilipofunguliwa kwa mara ya kwanza ,na hata  Novemba Mosi mwaka huu,kesi hiyo ilipokuja kwaajili ya kutajwa na wakili wa serikali Kweka aliieleza mahakama kuwa uplelezi wa shauri hilo umekamilika nilikuwepo tangu saa moja asubuhi mahakamani hapo, na  hata hiyo  Novemba 15 mwaka huu, panapo majaliwa ya mwenyezi mungu kesi hiyo itakapokuja kwaajili ya upane wa jamhuri kuwasomea maelezo ya awali washitakiwa nitakuwepo ndani ya ukumbi namba moja wa mahakama hiyo kwaajili ya kuiripoti kesi hiyo kwa uweledi wa aina yake.
Kwa mujibu wa hati ya mashitaka ya kesi hiyo inayomkabili Ponda na wenzake ambayo nakala yake ninayo, ina jumla ya mshitaka matano ambapo mashitaka yote matano yanamkabili Ponda na mashitaka manne yanamkabili mshitakiwa 2-50.
Kosa la kwanza  ni la kula njama kutenda kosa kinyume na kifungu cha  384 cha Sheri ya Kanuni ya Adhabu ya mwaka 2002, ambapo washitakiwa wote wanaidaiwa kuwa Oktoba 12 mwaka huu katika eneo la Chang’ombe  Marksi walikula njama kwania ya kutenda kosa.Kosa la pili ni  kuingia kwa nguvu  kwa nia ya kutenda kosa  kinyume na kifungu  cha 85,35 cha Sheria ya Kanuni ya Adhabu ,kuwa Oktoba 12 mwaka huu,  katika eneo la Chang’ombe Markasi ,kwa jinai na wasipokuwa na sababu  waliingia kwenye kiwanja cha eneo hilo kinachomilikiwa na Kiwanda cha Agritanza.
Wakati kosa la tatu ni  la kujimilikisha kwa jinai kiwanja hicho kinyume na kifungu cha 86 na 35 cha Sheria hiyo  kuwa kati ya Oktoba 12-16 mwaka huu, katika eneo hilo pasipo na uhalali washitakiwa wote  katika hali ya kupelekea uvunjifu wa amani,walijimilikisha  kwa nguvu ardhi ya kampuni ya Agritanza.
Shitaka la nne ni la wizi kinyume na kifungu cha 258 na 225 cha Sheria ya Kanuni ya Adhabu  ya mwaka 2002  kuwa washitakiwa wote kati ya Oktoba 12-16 mwaka huu, waliiba vifaa,malighafi  kama nondo,matofali ,kokoto zenye jumla ya Sh 59,650,000 mali ya Kampuni hiyo.
Aidha shitaka la tano ni kwaajili ya Ponda peke yake ambalo ni la uchochezi kinyume na kifungu cha 390 na 35 cha Sheria ya Kanuni  ya Adhabu  ya mwaka 2002 kuwa Oktoba 12 katika eneo hilo la Chang’ombe  kwa maelezo kuwa yeye ni Katibu  aliwashawishi wafuasi wake ambao ni washitakiwa hao watende makosa hayo.Na washitakiwa wote walikanusha mashitaka hayo na Hakimu Nongwa akasema mashitaka yote yanadhamana kwa mujibu wa sheria na akatoa masharti ya dhamana kwa mshitakiwa 2-50 .
Na kusema ili wapate dhamana nilazima kila mmoja awe na mdhamini mmoja wa kuaminika atakayesaini bondi ya milioni moja, licha Hakimu Nongwa alisema mahakama yake haiwezi kutoa dhamana kwa Ponda licha anastahili dhamana kwasababu Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP),Dk.Eliezer Feleshi aliwasilisha mahakamani hapo hati ya kufunga dhamana ya Ponda kwa mujibu wa kifungu cha 148(4) cha Sheria Mwenendo wa Makosa ya Jinai ya mwaka 2002.Na hati hiyo ya DPP inakuwa imeifunga mikono mahakama hadi hapo siku DPP atakapoona haja ya kuiondoa hati hiyo hivyo Ponda ataendelea kusota rumande hadi hati hiyo itakapoondolewa na DPP .
Kauli ya Profesa Lipumba kuhusu kesi ya Ponda imenifanya nianze kuamini kuwa hata ukiwa msomi wa hali ya juu kama Profesa Lipumba unaweza pia kutoa maoni ya kipuuzi ambayo hayapaswi kutolewa na msomi wa aina yake mbele ya umma.
Tumuulize huyu Lipumba kabla ya kutoa kauli hizo aliwasiliana na wanasheria wa chama chake wakampa ushauri wa kisheria wa nini cha kuzungumza mbele ya umma kuhusu kesi ya Ponda inayooendelea pale katika Mahakama ya Kisutu?Naamini hakupata ushauri  mzuri toka kwa wanasheria wa chama chake au kama alipata basi wanasheria huo waliamua kumpatia ushauri ambao umemdhalilisha Lipumba mbele ya jamii ya wasomi wa sheria na jamii inayoheshimu utawala wa sheria hapa nchini.
Profesa Lipumba kwanza kabla ya kutoa kauli hizo kuhusu kesi ya Sheikh Ponda kuwa kesi hiyo ya jinai namba 245 /2010 eti ilipaswa iwe ya jinai, ungeitafuta hati hati ya mashitaka ungeisoma vizuri na ungeweza kuelewa makosa wanayoshtakiwa nayo ni ya madai au jinai  halafu ungeenda kuisoma Sheria ya Kanuni ya Adhabu (Penal Code;2002),Sheria ya Mashauri ya Madai(Civil Procedure Code:2002) na Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai (Criminal Procedure Act, RE:2002) na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania naamini vingekupa mwongozo mzuri sana kwa kufahamu mashitaka yanayowakabili, kifungu gani kimetumika kufunga dhamana ya Ponda na ni kwanini dhamana yake imefungwa na pia ungeweza kufahamu vyema majukumu ya mahakama ni ya pili nay a serikali ni yapi.
Na hapo ndipo ninapokubaliana na kauli ya Rais Kikwete aliyoitoa mwishoni mwa wiki  ambayo inawataka wanasiasa waache unafki kwani wao wanaisasa wanaishi maisha kifahali na uhuru wakati wale wafuasi wao wanaishi maisha ya tabu na wamekuwa wakiwapandikisha uongo wafuasi wao.
Sasa kwa kauli hiyo ya Kikwete minaona katika matamko hayo ya Lipumba inamgusa pia, kwani uenda Lipumba anataka kujipatia umaarufu chee wa kisiasa kupitia kesi ya Ponda ila hafahamu kuwa mahakama haiendeshwi wala haisikilizi kauliza wanasiasa  pindi inapofanyakazi zake kwa mujibu wa sheria.
Wewe Lipumba kwakuwa unasema kesi ya jinai ya Ponda ilipaswa iwe ni ya madai, hivi ni kwanini unashindwa kuomba kazi ya kuwatetea washitakiwa hao kama (Bush Lawyer )mahakamani hapo na siku kesi ikianza kusikilizwa ukawasilisha hilo pingamizi lako lakutaka kesi hiyo ya jinai ifutwe kwani imefunguliwa kimakosa ilitakiwa washitakiwa hao wafunguliwe kesi ya madai).
Maana unapozungumzia kesi hiyo kwenye majukwaa na mbele ya waandishi wa habari haimsaidii Ponda kwa lolote zaidi zaidi unazidi kumgandamiza Ponda bila wewe kujua?
Profesa mzima tena wa uchumi unayeheshimika nchi mbalimbali unashindwa kufahamu mtu anayetuhumiwa kwa kosa la wizi au kuingia kwa nguvu kwenye kiwanja au chochezi basi mtu huyo makosa hayo yataangukia kwenye jamii ya makosa ya jinai? Lakini wewe sijui kwa upotoshaji au unalako jambo unadiriki kujitokeza adharani kuuposha umma kwa kusema walipaswa washitakiwe kwa kesi ya madai?
Mwenyekiti mzima wa chama kikubwa kama CUF,ambacho chama hicho chini ya uongozi wako ni miongoni mwa chama kilichokuwa kidai Tanzania iandike Katiba mpya kwa madai kuwa Katiba ya sasa imepitwa na wakati,na kwa maana hiyo unaifahamu vyema ibara za Katiba hiyo , unashindwa kuifahamu Katiba ya nchi ambayo Ibara ya 59B(1)  inayosomeka hivi; “Kutakuwa na Mkurugenzi wa Mashtaka  ambaye atateuliwa  na Rais,kutoka miongoni  mwa watu wenye  sifa zilizoanishwa  katika ibara ndogo (2) ya ibara  59 na amekuwa  na sifa hizo mfululizo kwa muad  usiopungua  miaka kumi.
Ibara ya 59(4) inasema; ‘Katika kutekeleza  mamlaka yake,Mkurugenzi wa Mashitaka  atakuwa huru ,hataingiliwa  na mtu yeyote  au mamlaka yeyote na atazingatia mambo yafuatayo; (a) nia ya kutenda haki, kuzuia matumuzi mabaya ya taratibu  za utoaji  haki na maslahi ya umma.
Na kifungu cha 148(4) cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya jinai, kina mpa mamlaka DPP kufunga dhamana ya mshitakiwa na ndiyo kifungu hicho kilichotumia na DPP kufunga dhamana ya Ponda.
Ni kweli dhamana ni haki ya kila mtu ila kuna baadhi ya makosa hayana dhamana na mfano kesi ya mauji, utakatishaji fedha haramu( Money Laundry),unyang’anyi wa kutumia silaha(Amry Robbery) mauji,uhaini na ugaidi (Terrorisms)  lakini kama kifungu hicho cha 148(4) cha Sheria ya Makosa ya Jinai, kinampa mamlaka DPP kumfungua dhamana mshitakiwa anayekabiliwa na makosa yanayodhaminika.
Sasa kwa mtiririko huo ,misimwelewi Lipumba ana ajenda gani iliyojificha kwenye hii kesi ya Ponda.Kwani Ponda na wenzake bado ni watuhumiwa kama wengine tub ado hajaukumiwa.DPP ametumia madaraka aliyonayo kufunga dhamana ya Ponda na  kuwafungulia mashitaka ya jinai washitakiwa hao ,sasa sijui tabu inatoka wapi.
Mbona viongozi wa iliyokuwa Taasisi ya Upatu (DECI) walivyofunguliwa kesi pale Mahakama ya Kisutu mwaka 2009, na makosa yanayowakabili yalikuwa yanadhaminika kwa mujibu wa sheria lakini  DPP huyu huyu Dk.Feleshi aliwasilisha hati ya kuwafungua dhamana na vigogo ambao kesi yao iliyopo mbele ya Hakimu Stewart Sanga imefikia hatua ya wao wameanza kujitetea,aliwafungia dhamana na walisota gerezani kwa zaidi ya miezi mitatu, mbona hatukuwasikia wanasiasa wala waumini wa dini ya Kikristo au wewe Lipumba na wale wafuasi wengine mnaondamana kila Ijumaa kushinikiza Ponda aachiliwe huru, hamkuandamana kushinikiza waachiliwe huru na kwamba kesi yao vigogo wa DECI ni ya madia?
Tuachane na uhuni huu unaofanywa na wasiasa waliopoteza dira na mwelekeo na waliofirisika kisiasa ambao wao masuala hatarishi na yanayoingilia uhuru wa mahakama ambao uhuru wa mahakama umeainishwa wazi katika Ibara ya 107B ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977, ambayo inasomeka hivi; “Katika kutekeleza mamlaka ya utoaji haki ,mahakama zote zitakuwa huru na zitalazimika kuzingatia  tu masharti ya Katiba na Sheria za Nchi’.
Na ibara 107A (1) ya Katiba ya nchi inasema “Mamlaka yenye mamlaka ya mwisho ya utoaji  haki katika jamhuri ya Muungano  itakuwa ni Mahakama.
Kwahiyo kama  kesi inayomkabili Ponda ni ya madai , si jukumu la wewe Lipumba sasa kusema hilo ni jukumu la Mahakama siku ikifika itasema hivyo.
Mwisho napenda kuwaasa wale wanaojiita wafuasi wanaojiita wao ni wafuasi wa  Ponda na sheikh Farid waache kushiriki kwenye vitendo vya uvunjifu wa amani kwa kisingizo cha kuishinikiza serikali na mahakama imwachilie huru Ponda kwani kufanya hivyo ni wazi wakae wakijua watakuwa wanafunja sheria za nchi watajikuta wanaingia matatani na wao waishia kwa kufunguliwa kesi za jinai mahakamani na kutupwa jela.
Na wale wahuni wachache ambao ni wazi wamechoka kuishi Tanzania kwenye amani wanaoleta vurugu za kidini kwa kisingizio eti wanaitetea dini ya kiislamu, wakome mara moja na kwa uwezo wa mungu hiyo dhamira yao mbaya na kishetani ya kutaka kuingiza Tanzania kwenye machafuko haitafanikiwa nao mwisho wa siku wataambulia kipigo kutoka kwa wanausalama wetu na kufikishwa mahakamani na mwishowe kupelekwa kupumzika katika gereza la Segerea,Keko na kula ugali wa bure na kuwa chini ya ulinzi.
Naendelea kuvipongeza vyombo vyetu vya ulinzi na usalama kwa kazi nzuri wanayoifanya ya kuwadhibiti wahuni hawa wachache wanajaribu kutaka kuatarisha usalama wa taifa letu kwa visingizio visivyokuwa na kichwa wala miguu.Na ninaviomba vyombo vya dola viwashughulikie kikamilifu wale wote wanaoleta vurugu kwa kisingizio cha kutetea dini ya kiislamu wakati bado wakristo,waislamu na wapagani hapa nchini tunaishi kwa upendo,tunafanyakazi pamoja.
Mwisho nimalizie kwa kuwataka waandishi wa habari wenzangu na wanaharakati na wanasiasa ambao huko nyuma tulikuwa mstari wa mbele sana kushikilia bango hadi kuandaa maandamano na kutengeneza mabango na fulani za kulaani tuhuma za ufisadi katika Mkataba wa Dowans,Richmond, mauji ya mwanahabari mwenzetu David Mwangosi,kufungiwa kwa vyombo mbalimbali vya habari.
Mbona wanahabari wenzangu wengi,wanaharakati,na wanasiasa machahari mbona tumeonekana kuwa wapole sana katika matukio haya yanayotaka kuleta chochoko za kidini? 
Hivi  je matukio haya yanayoashiria chokochoko ya udini siyana madhara ya haraka,wazi ambayo yasingezibitiwaharaka na vyombo vya dola na hekima ya viongozi wa dini ya Kikristo na wale wa kiislamu leo hii Tanzania ingekuwa imeingia kwenye machafuko ya kidini?
Tuache unafki,amani ni kitu muhimu sana pote pale duniani na chenye kipaumbele halafu hayo mambo mengine yanafuata.Kwani bila ya kuwepo na amani huo ufisadi usingenyika.
Mungu ibariki Tanzania, Mungu Ibariki Afrika
0716 774494
 
 
Mwisho wa makala yake, chadema wanasemaje juu ya kadhia hiyo?
 
 

Chadema waweka bayana msimamo wao juu yaliowasibu ma-shiekh


Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kimekutana na waandisihi wa habari makao makuu ya chama hicho jijini Dar es Salaam leo, ambapo wajumbe wa Kamati Kuu, Profesa Abdallah Safari na Mabere Marando, wameweka waziwazi msimamo wa chama hicho kuhusiana na mgogoro kati ya waislamu na serikali na kukamatwa kwa Sheikh Farid huko Zanzibar.
Wanasheria hao wa CHADEMA wamesema kuwa kitendo cha serikali kumnyima dhamana Sheikh Ponda ni kinyume cha katiba na kwamba Chadema kama chama kinachojiandaa kuchukua dola, hakiwezi kuvumilia kuona haki za raia zikivunjwa.
“Tunaweza kuwa miongoni mwetu, wapo watu wanaomchukia Sheikh Ponda, lakini hatuwezi kuficha ukweli kwamba Sheikh Ponda kama raia wa Jamhuri ya Muungano au mkazi wa Jamhuri hii, anayo haki ya kusikilizwa na kupewa dhamana. Makosa ambayo Sheikh Ponda ameshitakiwa yanadhaminika kwa mujibu wa sheria, hivyo ni makosa kwa serikali kufanya hila kumnyima dhamana kiongozi huyu wa kidini,” ameeleza Marando katika mkutano huo.
Marando alifika mbali zaidi kwa kusema tatizo lililopo sasa kati ya serikali na waislamu, limetokana na hatua ya serikali kuwalazimisha waislamu wote kuwa waumini wa Bakwata, chombo ambacho wengi wanakiona kinatumika kuwakandamiza.
Naye Profesa Safari alionya matumizi ya nguvu za kijeshi yanayotumiwa na serikali kwa kisingizio cha kulinda amani, huku akieleza kuwa matumizi ya kijeshi siyo suluhu ya kutatua matatizo yaliopo.
Kuhusu kukamatwa kwa Sheikh Faridi na kumzuia kwa siku tatu, wanasheria hao wamesisitiza kuwa kitendo hicho hakikubaliki.
“Kitendo cha kumkamata na kumshikiria Sheikh Faridi, huku serikali na vyombo vyake vikisema havihusiki, wakati ukweli ni kuwa alikuwa anashikiliwa na watu wa USALAMA wa TAIFA, ni uharamia mkubwa unaopaswa kulaaniwa na wote wanaolitakia mema taifa hili,” ameeleza Marando.
Kuhusu uvunjwaji wa makanisa, Profesa Safari amesema CHADEMA kimelaani hatua hiyo iliyotokana na wananchi kujichukulia sheria mkononi. Amewataka waislamu kuvuta subira.
Hata hivyo, Profesa Safari amesena matatizo yanayotokea sasa, yameletwa na CCM kutokana na hatua yao ya kuwatumia baadhi ya waislamu kupandikiza mbegu ya udini nchini.
Chanzo Chadema Blog

Mwisho wa msimamo wa chadema, unaofuata ni msimamo wa cuf uliotolewa na Prof Ibrahim Haruna Lipumba.



                THE CIVIC UNITED FRONT                       (CUF –Chama Cha Wananchi)

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI KUHUSU JUHUDI ZA CUF ZA KUENDELEZA AMANI NA UTULIVU BAADA YA SALA YA IJUMAA TAREHE 2 NOVEMBA 2012

Siku ya Alhamis nikielekea Muhimbili kumpeleka shangazi yangu hospitali nilipata taarifa kuwa Imam wa msikiti wa Masjid Haq (ulioko jirani na Afisi Kuuya CUF na ambapo nasali sala ya Ijumaa nikiwa Afisi Kuu) na watu wengine watatu akiwemo Sheikh Ramadhan S. Sanze (ambaye namfahamu kwa muda mrefu). Sadik Gogo na Mzee Abdillah wamekamatwa na wamefikishwa kituo cha polisi cha kati (Central Police Station). Nilistushwa na kamata kamata hiina nikahofia kuwa inaweza kuongeza jazba miongoni mwa waumini wa Kiislam. Baada ya shangazi kupata tiba katika hospitali ya Muhimbili nilimrudisha nyumbani na nikampigia simu Mkurugenzi wa Haki za Binadamu na mahusiano ya umma, Abdul Kambaya, tukutane kituo cha polisi cha kati kuulizia sababu za kukamatwa Imam wa MasjidHaq na wenzake watatu na kama tunaweza kuwawekea dhamana.Tulipof ika kituo cha polisi tulibaini kuwa Imam wa Msikiti wa Masjid Haq hajakamatwa bali kuna muumini mwingine kwa jina la Mkadam Swalehe ndiye aliyekamatwa. Tulizungumza na RPC Kova na RCO Msangi kuhusu kuachiliwa kwa wale waliokamatwa. Tukafahamishwa kuwa itabidi wafanyiwe mahojiano na baadaye wataachiliwa isipokuwa Mkadam Swalehe ambaye ana faili jingine pale polisi linaloendelea kufanyiwa upelelezi. Tulifahamishwa kuwa nitume mtu saa 10:30 jioni ili aweze kufuatilia utaratibu wa kuachiliwa watuhumiwa watatu akiwemo Sheikh Ramadhan Sanze, Sadik Gogo na Mzee Abdillah.Nilish auriana na Wakurugenzi wa CUF walioko Dar es Salaam na Naibu Katibu Mkuu, Julius Mtatiro hatua za kuchukua. Taarifa za kukamatwa Sheikh Ramadhan Sanze na wenzake zilikuwa zinaenea na kupandisha jazba ya Waislam wengi. Tulipata wasiwasi kuwa jazba hii inaweza kupelekea Waislam wengi kuandamana baada ya sala ya Ijumaa.Ikiwa Sheikh Ramadhan Sanze na wenzake wataachiwa na Waislam wakapata taarifa hiyo inaweza kusaidia kupunguza jazba na watu wasishiriki maandamano baada ya sala ya Ijumaa.Nilimpa jukum Abdul Kambaya afuatilie Central PoliceStation, suala la kuachiliwa Sheikh Sanze na wenzake. Niliwasiliana naye kwa simu na kuzungumza na RCO na nikaamini kuwa Sheikh Ramadhan Sanze, Sadik Gogo na Mzee Abdillah wataachiwa baada ya kukamilishamaho jiano. Ilikuwa inakaribia saa 12 jioni. Muda wa kuitisha Press Conference haukuwepo. Tukakubaliana Naibu Katibu Mkuu awasiliane na wahariri wa habari wa vituo vya televisheni Channel10, TBC1, Star TV, Mlimani TV na ITV ili niweze kutoa taarifa ya kuwasihi Waislam warudi majumbani na kwenye shughuli zao baada ya sala ya Ijumaa. Niliweza kufanya mahojiano na Channel 10, TBC1, na ITV. Kwa bahati mbaya Camera person wa Star TV alikuwa kwenye shughuli nyingine na kwa hiyo sikuweza kufanya mahojiano na Star TV. Vilevile wapiga picha wa Mlimani TV hawakuwepo kwenye studio. Pia nilipatabahati ya kuzungumza na Radio Iman inayosikilizwa na Waislam wengi na kueleza maoni yangu kuwa Waislam wasiandamane baada ya sala ya Ijumaa.Baada ya kutoa taarifa kwenye vituo vitatu vya televisheni na Radio Iman kuwa Sheikh Ramadhan Sanze na wenzake wataachiliwa na kuwasihi Waislam wasishiriki maandamano baada ya sala ya Ijumaa nilimpigia simu Abdul Kambaya kuulizia kama naweza kuzungumza na Sheikh Ramadhan Sanze. Kambaya akanieleza mambo yamebadilikana hawajaachiwa. Niliwasiliana na RCOna nikabaini kuwa suala hilo haliko tena chini ya uamuzi wake na litakamilishwa siku ijayo.Usiku wa alhamisi kuamkia Ijumaa nilijaribu kuwasiliana na Rais Kikwete kupitia wasaidizi wake ili nimfahamishe mantiki na sababu ya hatua nilizochukua na atumie uwezo wake alionao Sheikh Ramadhan Sanze na wenzake waachiliwe. Kwa bahati msaidizi mmoja alipata ujumbe wangu wa simu na akanipigia simu saa 6:50 usiku na kunifahamisha atajitahidi kuufikisha ujumbe wangu kwa Mhe. Rais ili nipate kuongea naye kuhusu jamaa wanaoshikiliwa na polisi waachiwe ili kupunguza jazba na kuepusha shari. Niliyezungumza naye alikuwa Dodoma na Rais alikuwa Arusha na ratiba yake ilikuwa imebana sana na kwa hiyo hakuweza kupata fursa ya kunipigia simu siku hiyo ya Ijumaa.Siku ya Ijumaa Abdul Kambaya aliendelea kufuatilia kuachiwa kwa Sheikh Ramadhan Sanze na wenzake Central Police Station. Nami katika kuhangaika ili waliokamatwa waachiliwe nilipata fursa ya kuzungumza na IGP na kumfahamisha sababu ya juhudi nilizochukua na mategemeo yangu kuwa Sheikh Sanze na wenzake wangeachiwa. Ninakiri kuwa katika mazungumzo ya simu, IGP Mwema alikuwa msikivu na mkarimu sana katika kauli yake. Alinishukuru kwa kauli niliyoitoa katika vituo vya televisheni na kuwa atafuatilia suala nililomueleza. Hatimaye Sheikh Ramadhan Sanze na wenzake waliachiwa.Naam ini kama Sheikh Ramadhan Sanze na wenzake wangeachiwa ingesaidia sana kupunguza jazba. Hata hivyo Waislam wengi na wananchi wengine kwa ujumla walipokea vizuri wito wangu na hawakushiriki katika maandamano. Baadhi wamenikosoa na kushauri kuwa ilifaa nisubiri mpaka baada ya maandamano kufanyika na kama patatokea majeruhi na vifo ndipo nitoe tamko la kulaani vitendo vya polisi na serikali.Katika mitandao ya kijamii wengine wamekejeli juhudi zangu. Nilikubali kushiriki katika kipindi cha Makutano show kinachoendeshwa na Bi. Fina ambapo hupata maswali toka Jamii Forum. Moja ya swali lililotolewa ni “Muulize very very solid, kuna agenda gani kati ya Cuf na uislam? mtaani leo wanasema kauli ya Lipumba ya jana kusitisha maandamano wameitii, na ukiangalia mikutano yake pale jangwani utafikiri kuna mawaidha ni balaghashia na baibui.” Fina hakupata muda wa kuniuliza swali hili. Jibu lake ni la wazi. CUF inasimamia Haki Sawa kwa Wananchi Wote. Kuna Watanzania wengi ambao ni Waislam na wao pia wanastahiki kutendewa haki katika nchi yao. Kuhusu balaghashia na baibui ni vyema vijana wakatazama picha za umati wa watu uliokuwa unahutubiwa na Mwalimu Nyerere wakati wa kupigania uhuru wa nchi hii. Picha hizo pia zinaonyesha waliokuwa wakipigania uhuru wengi walivaa balaghashia na baibui hata Mwalimu Nyerere alipewa zawadi nyingi za balaghashia na akaamua kuzivaa. Kushamiri kwa demokrasia ya kweli msingi wake mkubwa ni amani na utulivu. Amani ya kweli haipatikani bila kuwepo haki. Kesi ya Sheikh Ponda msingi wake na madai ya kiwanja. Ki msingi kesi ya madai ya kusuluhishwa na Mahakama ya ardhi. Sheikh Ponda ana haki ya msingi ya kupewa dhamana hata kama kauli zake haziifurahishi serikali.Nasiki tika sana katika kipindi hiki tete,viongozi wa serikali wameshindwa kuchukua juhudi za makusudi kuzungumza na Maimam wa misikiti na viongozi wa asasi za Kiislam kupunguza jazba. Badala yake wameachia kauli za vitisho vya Kamanda Kova ndiyo viwe mawasiliano kati ya serikali na Waislam.Ni vyema serikali ikatumia busara na kuwasiliana na Maimamu wa misikiti na viongozi wa asasi za Kiislam kuelewa hoja na malalamiko yao.Hatimaye nimepata fursa ya kuzungumza na Mheshimiwa Rais leo asubuhi na nikamueleza juhudi nilizozichukua kuweza kupunguza jazba na kuwaomba Waislam wasishiriki kwenye maandamano baada ya sala ya Ijumaa. Ni wazi hali hii ya mtafaruku ndani ya jamii inamsononesha sana Mheshimiwa Rais na ninaamini atajitahidi kwa uwezo wake wote kutafuta suluhisho.Katik a kutafuta suluhu ya mtafaruku huu nitaendelea na jitihada za kutafuta fursa niweze kubadilishana mawazo na Rais Kikwete. Nitazungumza na viongozi wa asasi za Kiislam. Nitazungumza na viongozi wa Makanisa ya Kikristo. Madhumuni ya mazungumzo yangu nikuwafahamisha mantiki ya juhudi nilizofanya na kushauriana misingi muhimu ya Waumini wote kuheshimiana na kuvumiliana ili tujenge Tanzania yenye haki sawa kwa wote.

Ibrahim Haruna Lipumba

Mwenyekiti
Novemba 4 2012
 
 
KWANINI ANATUKANWA PROF LIPUMBA PEKEE? HUHU MUANDISHI NI MBUMBU AU HANA AKILI TIMAMU?, WAANDISHI WENYE UPENDELEO WA DHAHILI NDIO WALIOSABABISHA MAUAJI YA KIMBALI RWANDA NA BURUNDI. WAANDISHI TUACHE UNAFKI.

Wabunge wataka Serikali tatu

(Kifupi: WAPENDEKEZA MAWAZIRI WASIWE WABUNGE, VITI MAALUMU VIFUTWE, URAIS MIAKA 35)
WABUNGE jana walijilipua baada ya baadhi yao kupendekeza kuwa muundo wa Muungano ubadilishwe kuwa wa Serikali tatu na kwamba, mawaziri wasiwe  wabunge.
Pamoja na mapendekezo hayo, wengine walitaka umri wa kugombea urais ushushwe na kuwa miaka 35, badala ya sasa ya miaka 45.
Wakitoa maoni yao kwa Tume ya Mabadiliko ya Katiba inayoongozwa na Jaji Joseph Warioba mjini Dodoma jana, wabunge hao pia walitaka viti maalumu vya ubunge vifutwe, badala yake wanawake warejee kugombea ubunge majimboni.
Katika mkutano huo, zaidi ya wabunge 36 walitumia nafasi hiyo kutoa maoni yao kuhusu masuala mbalimbali yenye masilahi kwa taifa, waliyoona yanafaa kuingizwa kwenye Katiba Mpya, ambayo mchakato wa ukusanyaji maoni ya uundwaji wake, unaendelea.
Muungano
Mbunge wa Viti Maalumu (CCM), Ester Bulaya alitaka muundo wa muungano ubadilishwe na kuwa wa Serikali tatu, badala ya uliopo sasa aliosema una kasoro nyingi.
Moja ya kasoro hiyo ni wawakilishi kuruhusiwa kuingia katika Bunge la Jamhuri ya Muungano, huku wabunge wa Bara wakiwa hawana uwakilishi katika Baraza la Wawakilishi.
“Mwenyekiti, tuwe na Serikali tatu katika muungano, vinginevyo kila mmoja abaki na chake," alisema.
Pia alitaka viti maalumu vifutwe, badala yake wanawake wawekewe majimbo ya wilaya, ambayo watagombea na wenzao.
Mbunge wa Kilindi (CCM), Beatrice Shelukindo naye alitaka muundo wa muungano uwe wa Serikali tatu pamoja na kuruhusiwa kwa mgombea binafsi katika  nafasi mbalimbali.
Alisema kuwa mawaziri, wakuu wa mikoa na wakuu wa wilaya wasitokane na wabunge kwa sababu hawataweza kufanya kazi kwa ufanisi na ni mgongano wa kimasilahi.
Mbunge wa Mkanyangeni (CUF), Mohamed Mnyaa alitaka kuwapo na Serikali tatu katika muungano.
Alisema kama Tanzania Bara watakataa kuita nchi yao Tanganyika basi wanaweza kuiita jina lolote hata Mzizima.
“Muungano uwe wa Serikali tatu, Tanganyika wawe na nchi yao na sisi tuwe na Zanzibar yetu, kama bara hawataki kuiita nchi yao Tanganyika basi wanaweza kuiita hata Mzizima,”  alisema.
Kwa upande wake Mbunge wa Chakechake, (CUF), Mussa Haji Kombo alitaka muundo wa Muungano uliopo ubadilishwe badala yake uwe wa mkataba.
Chanzo: mwananchi

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI KUHUSU JUHUDI ZA CUF ZA KUENDELEZA AMANI NA UTULIVU BAADA YA SALA YA IJUMAA TAREHE

Mwenyekiti Cuf Taifa - Prof Ibrahim Haruna Lipumba
THE CIVIC UNITED FRONT
(CUF – Chama Cha Wananchi)
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI KUHUSU JUHUDI ZA CUF ZA KUENDELEZA AMANI NA UTULIVU BAADA YA SALA YA IJUMAA TAREHE 2 NOVEMBA 2012
Siku ya Alhamis nikielekea Muhimbili kumpeleka shangazi yangu hospitali nilipata taarifa kuwa Imam wa msikiti wa Masjid Haq (ulioko jirani na Afisi Kuu ya CUF na ambapo nasali sala ya Ijumaa nikiwa Afisi Kuu) na watu wengine watatu akiwemo Sheikh Ramadhan S. Sanze (ambaye namfahamu kwa muda mrefu). Sadik Gogo na Mzee Abdillah wamekamatwa na wamefikishwa kituo cha polisi cha kati (Central Police Station). Nilistushwa na kamata kamata hii na nikahofia kuwa inaweza kuongeza jazba miongoni mwa waumini wa Kiislam. Baada ya shangazi kupata tiba katika hospitali ya Muhimbili nilimrudisha nyumbani na nikampigia simu Mkurugenzi wa Haki za Binadamu na mahusiano ya umma, Abdul Kambaya, tukutane kituo cha polisi cha kati kuulizia sababu za kukamatwa Imam wa Masjid Haq na wenzake watatu na kama tunaweza kuwawekea dhamana.
Tulipofika kituo cha polisi tulibaini kuwa Imam wa Msikiti wa Masjid Haq hajakamatwa bali kuna muumini mwingine kwa jina la Mkadam Swalehe ndiye aliyekamatwa. Tulizungumza na RPC Kova na RCO Msangi kuhusu kuachiliwa kwa wale waliokamatwa. Tukafahamishwa kuwa itabidi wafanyiwe mahojiano na baadaye wataachiliwa isipokuwa Mkadam Swalehe ambaye ana faili jingine pale polisi linaloendelea kufanyiwa upelelezi. Tulifahamishwa kuwa nitume mtu saa 10:30 jioni ili aweze kufuatilia utaratibu wa kuachiliwa watuhumiwa watatu akiwemo Sheikh Ramadhan Sanze, Sadik Gogo na Mzee Abdillah.
Nilishauriana na Wakurugenzi wa CUF walioko Dar es Salaam na Naibu Katibu Mkuu, Julius Mtatiro hatua za kuchukua. Taarifa za kukamatwa Sheikh Ramadhan Sanze na wenzake zilikuwa zinaenea na kupandisha jazba ya Waislam wengi. Tulipata wasiwasi kuwa jazba hii inaweza kupelekea Waislam wengi kuandamana baada ya sala ya Ijumaa. Ikiwa Sheikh Ramadhan Sanze na wenzake wataachiwa na Waislam wakapata taarifa hiyo inaweza kusaidia kupunguza jazba na watu wasishiriki maandamano baada ya sala ya Ijumaa.
Nilimpa jukum Abdul Kambaya afuatilie Central PoliceStation, suala la kuachiliwa Sheikh Sanze na wenzake. Niliwasiliana naye kwa simu na kuzungumza na RCO na nikaamini kuwa Sheikh Ramadhan Sanze, Sadik Gogo na Mzee Abdillah wataachiwa baada ya kukamilisha mahojiano. Ilikuwa inakaribia saa 12 jioni. Muda wa kuitisha Press Conference haukuwepo. Tukakubaliana Naibu Katibu Mkuu awasiliane na wahariri wa habari wa vituo vya televisheni Channel 10, TBC1, Star TV, Mlimani TV na ITV ili niweze kutoa taarifa ya kuwasihi Waislam warudi majumbani na kwenye shughuli zao baada ya sala ya Ijumaa. Niliweza kufanya mahojiano na Channel 10, TBC1, na ITV. Kwa bahati mbaya Camera person wa Star TV alikuwa kwenye shughuli nyingine na kwa hiyo sikuweza kufanya mahojiano na Star TV. Vilevile wapiga picha wa Mlimani TV hawakuwepo kwenye studio. Pia nilipata bahati ya kuzungumza na Radio Iman inayosikilizwa na Waislam wengi na kueleza maoni yangu kuwa Waislam wasiandamane baada ya sala ya Ijumaa.
Baada ya kutoa taarifa kwenye vituo vitatu vya televisheni na Radio Iman kuwa Sheikh Ramadhan Sanze na wenzake wataachiliwa na kuwasihi Waislam wasishiriki maandamano baada ya sala ya Ijumaa nilimpigia simu Abdul Kambaya kuulizia kama naweza kuzungumza na Sheikh Ramadhan Sanze. Kambaya akanieleza mambo yamebadilika na hawajaachiwa. Niliwasiliana na RCO na nikabaini kuwa suala hilo haliko tena chini ya uamuzi wake na litakamilishwa siku ijayo.
Usiku wa alhamisi kuamkia Ijumaa nilijaribu kuwasiliana na Rais Kikwete kupitia wasaidizi wake ili nimfahamishe mantiki na sababu ya hatua nilizochukua na atumie uwezo wake alionao Sheikh Ramadhan Sanze na wenzake waachiliwe. Kwa bahati msaidizi mmoja alipata ujumbe wangu wa simu na akanipigia simu saa 6:50 usiku na kunifahamisha atajitahidi kuufikisha ujumbe wangu kwa Mhe. Rais ili nipate kuongea naye kuhusu jamaa wanaoshikiliwa na polisi waachiwe ili kupunguza jazba na kuepusha shari. Niliyezungumza naye alikuwa Dodoma na Rais alikuwa Arusha na ratiba yake ilikuwa imebana sana na kwa hiyo hakuweza kupata fursa ya kunipigia simu siku hiyo ya Ijumaa.
Siku ya Ijumaa Abdul Kambaya aliendelea kufuatilia kuachiwa kwa Sheikh Ramadhan Sanze na wenzake Central Police Station. Nami katika kuhangaika ili waliokamatwa waachiliwe nilipata fursa ya kuzungumza na IGP na kumfahamisha sababu ya juhudi nilizochukua na mategemeo yangu kuwa Sheikh Sanze na wenzake wangeachiwa. Ninakiri kuwa katika mazungumzo ya simu, IGP Mwema alikuwa msikivu na mkarimu sana katika kauli yake. Alinishukuru kwa kauli niliyoitoa katika vituo vya televisheni na kuwa atafuatilia suala nililomueleza. Hatimaye Sheikh Ramadhan Sanze na wenzake waliachiwa.
Naamini kama Sheikh Ramadhan Sanze na wenzake wangeachiwa ingesaidia sana kupunguza jazba. Hata hivyo Waislam wengi na wananchi wengine kwa ujumla walipokea vizuri wito wangu na hawakushiriki katika maandamano. Baadhi wamenikosoa na kushauri kuwa ilifaa nisubiri mpaka baada ya maandamano kufanyika na kama patatokea majeruhi na vifo ndipo nitoe tamko la kulaani vitendo vya polisi na serikali.
Katika mitandao ya kijamii wengine wamekejeli juhudi zangu. Nilikubali kushiriki katika kipindi cha Makutano show kinachoendeshwa na Bi. Fina ambapo hupata maswali toka Jamii Forum. Moja ya swali lililotolewa ni “Muulize very very solid, kuna agenda gani kati ya Cuf na uislam? mtaani leo wanasema kauli ya Lipumba ya jana kusitisha maandamano wameitii, na ukiangalia mikutano yake pale jangwani utafikiri kuna mawaidha ni balaghashia na baibui.” Fina hakupata muda wa kuniuliza swali hili. Jibu lake ni la wazi. CUF inasimamia Haki Sawa kwa Wananchi Wote. Kuna Watanzania wengi ambao ni Waislam na wao pia wanastahiki kutendewa haki katika nchi yao. Kuhusu balaghashia na baibui ni vyema vijana wakatazama picha za umati wa watu uliokuwa unahutubiwa na Mwalimu Nyerere wakati wa kupigania uhuru wa nchi hii. Picha hizo pia zinaonyesha waliokuwa wakipigania uhuru wengi walivaa balaghashia na baibui hata Mwalimu Nyerere alipewa zawadi nyingi za balaghashia na akaamua kuzivaa.
Kushamiri kwa demokrasia ya kweli msingi wake mkubwa ni amani na utulivu. Amani ya kweli haipatikani bila kuwepo haki. Kesi ya Sheikh Ponda msingi wake na madai ya kiwanja. Ki msingi kesi ya madai ya kusuluhishwa na Mahakama ya ardhi. Sheikh Ponda ana haki ya msingi ya kupewa dhamana hata kama kauli zake haziifurahishi serikali.
Nasikitika sana katika kipindi hiki tete, viongozi wa serikali wameshindwa kuchukua juhudi za makusudi kuzungumza na Maimam wa misikiti na viongozi wa asasi za Kiislam kupunguza jazba. Badala yake wameachia kauli za vitisho vya Kamanda Kova ndiyo viwe mawasiliano kati ya serikali na Waislam. Ni vyema serikali ikatumia busara na kuwasiliana na Maimamu wa misikiti na viongozi wa asasi za Kiislam kuelewa hoja na malalamiko yao.
Hatimaye nimepata fursa ya kuzungumza na Mheshimiwa Rais leo asubuhi na nikamueleza juhudi nilizozichukua kuweza kupunguza jazba na kuwaomba Waislam wasishiriki kwenye maandamano baada ya sala ya Ijumaa. Ni wazi hali hii ya mtafaruku ndani ya jamii inamsononesha sana Mheshimiwa Rais na ninaamini atajitahidi kwa uwezo wake wote kutafuta suluhisho.
Katika kutafuta suluhu ya mtafaruku huu nitaendelea na jitihada za kutafuta fursa niweze kubadilishana mawazo na Rais Kikwete. Nitazungumza na viongozi wa asasi za Kiislam. Nitazungumza na viongozi wa Makanisa ya Kikristo. Madhumuni ya mazungumzo yangu ni kuwafahamisha mantiki ya juhudi nilizofanya na kushauriana misingi muhimu ya Waumini wote kuheshimiana na kuvumiliana ili tujenge Tanzania yenye haki sawa kwa wote.

Ibrahim Haruna Lipumba
Mwenyekiti
Novemba 4 2012

Sunday, September 23, 2012

CHADEMA IMEDANDIA BEHEWA LA CUF!

Naibu katibu Mkuu JUVICF-Thomas Malima

Wengi tunaamini kuwa Elimu ni ufunguo wa maisha. Waandishi wamesomeshwa kwa kodi za watanzania kwa lengo la kupata elimu ya kuwahabarisha watanzania habari za ukweli na uhakika juu ya mustakabali wa maisha yao.

Lengo la elimu ni kujenga uwezo wa mambo makuu matatu kwa kila mwananchi ambayo ni uwezo wa kuhoji au kuuliza, uwezo wa kujifunza na uwezo wa kujiamini. Katika haya yote mkazo upo katika ubora na si vinginevyo, yaani kumjenga msomaji hasa mwandishi uwezo wa kufikiri, kusikiliza, kuuliza maswali, kupambanua na kuwasiliana na jamii bila kupotosha.

Baadhi ya waandishi wa habari nchini hawana uwezo uliotajwa hapo juu kutokana na kuandika makala zisizo na utafiti wala umakini kwa umma. Makala iliyoandikwa na mwandishi Mashaka Mgeta katika gazeti la Nipashe la tarehe 19 Septemba 2012 yenye kichwa CUF INAPOPANDIA BEHEWA LA CHADEMA ni ya kishabiki na yenye lengo la kuudanganya umma na zaidi ya yote imemdhalilisha mwandishi huyo pamoja na mhariri wa gazeti hilo kwa kuandika habari zisizo za utafiti.

CUF ilianza kauli mbiu yake ya VISION FOR CHANGE  mwaka 2008 na kuiweka rasmi kwenye Manifesto yake ya uchaguzi ya mwaka 2010. Tangu mwaka huo CUF haikuwahi kubadili kauli mbiu hiyo hadi wakati huu. Lakini cha kushangaza ni pale CHADEMA walipodandia kauli mbiu hiyo kwa kuzindua Movement for change M4C mwaka 2011. Ikumbukwe kuwa CUF iliinadi V4C nchi nzima wakati wa kampeni za uchaguzi za mwaka 2010 lakini leo baadhi ya waandishi wanajaribu  kuupotosha umma wa Watanzania kuwa CUF imedandia M4C ya CHADEMA. Je kwa ushahidi huo kati ya CUF na CDM nani amedandia hoja ya mwingine­­­­­?.

Hili si jambo la kwanza kwa CDM kuiga kutoka kwa CUF. Watanzania watakumbuka kuwa rangi za mwanzo za bendera ya CHADEMA  zilikuwa ni BLUE NA NYEUPE lakini baada ya kuona bendera za CUF zinavutia na zinaashiria mabadiliko ya kweli waliziiga na hatimaye kubadilisha bendera ya Chama chao ili zifanane na CUF kwa lengo la kuwatapeli wanachama na wafuasi wa CUF mikoani kuwa wao na CUF ni kitu kimoja hivyo wawape ushirikiano kwani wote ni wapinzani wa CCM.

CHADEMA pia waliendelea kuiga kauli  mbiu iliyokuwa inatumiwa na viongozi wa CUF kwenye mikutano yao. Watanzania watakumbuka kuwa  kaulimbiu ya mwanzo ya CHADEMA ilikuwa CHADEMA ……VEMA huku wakinyanyua vidole viwili. Lakini katika mkutano wa CUF kama chama kikuu cha upinzani kilichokuwa kinalea vyama vingine vidogo ikiwamo CHADEMA pale Viwanja vya BAKHRESSA mwaka 2004 ndipo aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wa CUF Zanzibar mheshimiwa Juma Duni alipozindua kauli mbiu ya NGUVU YA UMMA….CHACHU YA MABADILIKO. Baada ya mkutano huo ulioshirikisha vyama vingine kama CHADEMA ndipo Viongozi wa CHADEMA walipoamua kubadilisha kauli mbiu yake kuwa PEOPLES …..POWER. Iweje leo watu wasahaulishwe ukweli wa nani si mbunifu na nani anayesubiria mwingine abuni ili yeye aje na kukopi?.

Watanzania watakumbuka kuwa tangu CUF ilipoanzishwa ilikuwa na hoja ya Tanzania kuwa serikali 3 wakati CHADEMA ilikuwa inadai serikali ya MAJIMBO. Lakini cha kushangaza leo hii CHADEMA wamehama katika hoja yao ya Serikali ya majimbo na kuanza kuibaka hoja ya CUF ya serikali 3. Je hili nalo hamulioni kuwa CHADEMA hawana jipya bali wanasubiri CUF waibue hoja na wao ndo wanaibukia juu kwa juu?.

Suala mahitaji ya Katiba Mpya nalo limeonesha kuwa CUF ndicho chama pekee kilicho kinara cha Mabadiliko nchini maana CUF imesimamia suala hilo tangu kuasisiwa kwake hadi leo. WanaCUF walifikia hatua ya kufyatuliwa Risasi za Moto na kuwaangamiza zaidi ya wanaCUF 40 nchi nzima. Lakini leo juhudi hizo zinaelekea kupotezwa. Ni CUF pekee ndiyo ilikuwa na agenda ya Katiba mpya tangu 1995 lakini CDM imekuja kujitokeza 2010 tu. Je hapa pia hawakudandia hoja ya CUF ya Katiba mpya?.

Watanzania watakumbuka kuwa Mwenyekiti wa CUF alipotoka Marekani mwanzoni mwa mwaka huu aliwaeleza watanzania namna ambavyo rasilimali za nchi hii zikitumika vizuri zinaweza kuleta mabadiliko na kuwanufaisha watanzania. Profesa Lipumba alisema hayo baada ya kufanya utafiti kwa muda wa miezi 6 nchini Marekani , ambapo alipendekeza kuwaomba wapenzi na wanachama wa vyama vya siasa kuchangia vyama vyao ili vipate nguvu ya kifedha itakayoleta mabadiliko kwa kuingoa CCM. Baada ya kutoa hotuba hiyo,CHADEMA waliamua kufanya harambee ya kuchangia chama chao mwanzoni mwa mwezi juni 2012. Cha ajabu CUF waliofanyia utafiti uchangiaji huo, walipoamua kuweka katika vitendo juzi, wanaCHADEMA wameibuka na kusema CUF imewaiga. Je, kati ya CUF iliyotumia miezi 6 kutafiti na CHADEMA walioiga baada utafiti wa CUF nani amedandia hoja ya mwingine?.

Mwisho napenda kutoa wito kwa watanzania kutambua kuwa kila wanachokiona kinafanywa na CUF leo kimefanyiwa utafiti wa kina na kuthibitika kuwa kinafaa. CUF itaendelea kuwa baba wa ubunifu kwa vyama vyingine. CHADEMA wataendelea kuiga kutoka kwa CUF maana viongozi wake bado ni wababaishaji na wapiga domo tu.


Thomas D.C Malima
                         
  Mwandishi wa makala hii ni Naibu Katibu Mtendaji wa Jumuiya ya vijana ya CUF-Chama cha Wananchi na anapatikana kwa simu namba 0715172256 na e-mail thommalima@yahoo.com.



Sunday, September 16, 2012

TANZANIA TUKO NYUMA SANA KATIKA USHINDANI WA KIUCHUMI WA KIMATAIFA

Mwenyekiti Cuf Taifa- Prof Ibrahim Lipumba

Taarifa ya kila mwaka inayotolewa na taasisi isiyokuwa ya kiserikali ya World Economic Forum (WEF) kuhusu ushindani wa kiuchumi wa mataifa(The Global Competitiveness Report 2012/13) inaonesha kuwa Tanzania imeshika nafasi ya 120 kati ya nchi 144 wakati nchi jirani ya Rwanda imeshika nafasi ya 63.
Nchi inayoongoza kwa ushindani wa kiuchumi wa mataifa ni Uswissi (Switzerland), ikifuatiwa na Singapore, Finland, Uswidi (Sweden), Uholanzi (Netherlands), Ujerumani, Marekani, Uingereza, Hongkong na Japan.
Katika nchi za Afrika inayoongoza kwa ushindani wa kiuchumi ni Afrika ya Kusini inayoshika namba ya 52, ikifuatiwa na Mauritius ambayo ni ya 54 na ya tatu ni Rwanda iliyoshika nafasi ya 63 katika orodha ya nchi 144.
Watafiti wa WEF wanaeleza kuwa ushindani wa uchumi wa taifa unatokana na asasi za uchumi na utawala, sera, raslimali na nguvukazi (raslimali watu) zinazobainisha kiwango cha tija katika uzalishaji wa bidhaa na huduma katika nchi na kwa hiyo kuiwezesha nchi kukuza uchumi kwa kasi, kuongeza utajiri wa nchi na neema kwa wananchi wake.
Ili kupima ushindani wa kiuchumi wa kila nchi, watafiti wamechunguza mambo ya msingi yanayochochea ukuaji wa uchumi na uletaji wa maendeleo kwa ujumla. Nchi zenye ushindani wa kiuchumi zinafanikiwa kuongeza ufanisi na tija katika uzalishaji wa bidhaa na usambazaji wa huduma. Zinatumia vizuri raslimali na nguvukazi na kwa hiyo kufanikiwa kukuza uchumi kwa muda mrefu. Katika ulimwengu wa utandawazi ambapo nchi zina fursa ya kuuza na kununua bidhaa na huduma katika soko la dunia ushindani wa kiuchumi ni nyenzo muhimu ya kuongeza kasi ya kukuza uchumi kwa kuvutia wawekezaji wa ndani na nje ya nchi.
Watafiti wa WEF wanaanda kielelezo (farihisi) cha ushindani wa uchumi wa mataifa. Kielelezo hiki kutunamia vigezo vingi kupima ushindani wa kiuchumi unaotokana na asasi, sera, raslimali na vipengele vingine ambavyo vinabainisha uwezo, ufanisi na kiwango cha tija katika uzalishaji mali wa sekta mbali mbali za uchumi na huduma. Kiwango cha tija na ufanisi katika uzalishaji ndicho kinachovutia uwekezaji wa ndani na nje na kuchochochea ukuaji wa uchumi na ongezeko la wastani la pato la kila mwananchi.
Utafiti wa WEF umebaini nguzo 12 za ushindani wa kiuchumi wa mataifa. Nguzo ya kwanza ni asasi za uchumi, utawala na sheria ambazo zinajenga mazingira ya kushirikiana katika shughuli za kiuchumi kwa mtu mmoja mmoja, kampuni na serikali katika shughuli za uzalishaji na kuongeza utajiri wa taifa. Umuhimu wa mfumo wa asasi ulio wazi na kufanya kazi kwa ufanisi na haki umebainika hata kwa nchi zilizoendelea baada ya mtikisiko na mgogoro wa sekta ya fedha ulioanza Marekani mwaka 2008 na kuikumba dunia yote. Ukosefu na udhaifu wa usimamizi wa asasi za fedha katika nchi zilizoendelea na hasa Marekani ndiyo chanzo cha kuporomoka na kuyumba kwa uchumi wa dunia kwa muda wa miaka minne iliyopita.
Ubora wa asasi za uchumi na utawala ni jambo la msingi katika ushindani wa kiuchumi wa kila taifa. Mfumo na utendaji wa asasi hizi ndiyo unaoshawishi uwekezaji wa vitega uchumi na uzalishaji wa bidhaa na huduma. Mfumo wa asasi ndiyo kigezo muhimu cha mgawanyo wa pato la taifa na gharama za utekeleza wa mikakati ya kukuza uchumi. Kwa mfano kuwepo kwa hakimiliki za kuaminika ni muhimu sana katika kushawishi uwekezaji. Ikiwa mali ya mtu inaweza kuporwa kwaurahisi na watu wengine au serikali, uwekezaji wa vitega uchumi utapungua.
Ubora wa mfumo wa asasi ni pamoja na kuwepo utawala bora, ufanisi katika shughuli na usambazaji wa huduma za serikali, kutokuwepo kwa rushwa, ukusanyaji mzuri wa kodi na uadilifu katika matumizi ya fedha za umma. Utendaji, ufanisi na maadili ya sekta binafsi yanachangia katika kujenga ushindani wa kiuchumi wa taifa husika.
Nguzo ya pili ya ushindani wa kiuchumi ni miundombinu. Miundombinu inayojumlisha usafiri- barabara, reli, bandari na viwanja vya ndege; ufuaji na usambazaji wa umeme; ugawaji na usambazaji wa maji; miundombinu ya majitaka, na miundombinu ya mawasiliano inayoharikisha upeanaji wa taarifa na habari. Ubora wa miundombinu unachangia sana katika kuongeza ufanisi na tija ili kukuza uzalishaji na kuchochea ukuaji wa uchumi.
Nguzo ya tatu ni utengamavu wa uchumi mpana (macroeconomic stability) kwa maana ya mfumko wa bei wa kadri, riba ziwe za nafuu na pasiwe na tofauti kubwa sana kati ya riba ya mikopo na riba wanaolipwa waweka akiba,  thamani ya sarafu iwe tengamavu na ya ushindani kwa wazalishaji wa bidhaa na huduma wa ndani ya nchi, akiba ya kutosha ya fedha za kigeni ya kuagizia bidhaa na huduma za nje, matumizi ya serikali yasizidi mapato ya serikali kwa kiasi kikubwa. Utengamavu wa uchumi mpana pekee haukuzi uchumi, bali unajenga mazingira ya kuvutia uwekezaji na ukuaji wa uchumi ikiwa mambo mengine kama vile miundombinu na asasi bora vipo. Kutokuwepo kwa utengamavu wa uchumi mpana kunaathiri motisha wa uwekezaji na uzalishaji kwani kunaweka mashaka makubwa kwa bei halisi za raslimali, nguvukazi, bidhaa na huduma mbalimbali.
Nguzo ya nne ni afya na elimu bora ya msingi. Wananchi wenye afya njema wana uwezo wa kufanya kazi kwa ufanisi na tija ya juu. Wananchi weye afya mbovu siyo wazalishaji wazuri. Afya duni inaongeza gharama za uzalishaji. Ubora wa elimu ya msingi kwa wananchi wote inawezesha wafanyakazi waweze kufundishika. Wafanyakazi wasiokuwa na elimu bora ya msingi na kujua kusoma vizuri siyo wepesi kujifunza teknolojia mpya ya uzalishaji.
Nguzo ya tano ni elimu na mafunzo ya juu. Elimu bora ya juu na hususan elimu ya sayansi na teknolojia ni muhimu kwa nchi zinazohitaji kuzalisha bidhaa zenye ubora wa hali ya juu na bidhaa za teknolojia. Katika ulimwengu wa utandawazi , kuwa na watu wenye elimu ya juu ya sayansi na teknolojia ni muhimu katika kujenga ushindani wa uzalishaji wa bidhaa za kisasa.
Nguzo ya sita ni ufanisi wa soko la bidhaa. Nchi zenye masoko ya bidha yenye ufanisi na ushindani halali yanavutia uwekezaji na uzalishaji wa bidhaa na huduma bora. Ushindani wa soko ni muhimu katika kumotisha uvumbuzi na ufanisi katika uzalishaji. Kodi za juu zinaondoa motisha na kuathiri ushindani wa kiuchumi. Katika soko ambalo wateja wake wana utamaduni wa kutaka bidhaa bora unasaidia kulazimisha kampuni zishindane katika kuzalisha bidhaa bora.
Nguzo ya saba ni ufanisi wa soko la ajira. Ufanisi na mnyumbuliko wa soko la ajira ni jambo la msingi katika kuhakikisha kuwa watu wanaajiriwa katika nyanja ambazo watakuwa na uzalishaji wenye tija kubwa kulingana na uwezo na ujuzi wao. Uchumi unaokua kwa kasi kubwa na kubadilika mfumo wake unahitaji wafanyakazi wapungue kwenye sekta zinazodidimia au kutoweka kabisa na waongezeke  katika sekta zinazokua kwa kasi. Bila kuwepo kwa mnyumbuliko wa soko la ajira, mabadiliko ya haraka ya mfumo wa uchumi kama vile kupungua kwa sekta ya kilimo na kuongezeka kwa sekta ya viwanda, hayawezi kutokea. Soko la ajira lenye ufanisi linawapa mishahara mizuri wafanyakazi hodari na makini ili kuwapa motisha wa kuendelea kuchapa kazi. Wafanyakazi wavivu na wazembe wanapata kipato kidogo ukilinganisha na wafanyakazi hodari. Wafanyakazi wote wanajua kuwa wakiendelea na uzembe watapoteza ajira.
Nguzo ya nane ni maendeleo ya soko la mitaji na huduma za fedha. Uchumi wa kisasa unahitaji huduma za mikopo na mitaji. Ukusanyaji wa akiba kwa ufanisi unaruhusu kuwepo kwa mikopo yenye riba nafuu. Akiba itumiwe vizuri kuwapa mikopo wazalishaji wenye tija ya juu. Benki na taasisi nyingine za fedha zina kazi ya kutambua wajasiriamali wenye miradi mizuri yenye tija na kuwakopesha mitaji. Kuwepo kwa benki na taasisi nyingine za fedha zinazofanya kazi kwa ufanisi kunachochea ukuaji wa uchumi.
Nguzo ya tisa ni utayari wa kiteknolojia. Katika ulimwengu wa utandawazi ambapo kuna mabadiliko ya mara kwa mara ya teknolojia ni muhimu kwa nchi kujenga uwezo wa wananchi na kampuni zilizomo nchini kupokea, kumudu na kutumia teknolojia mpya. Hivi sasa teknolojia ya habari na mawasiliano (TEHAMA) imekuwa na matumizi katika nyanja zote za uzalishaji, elimu, afya na huduma nyingine. Taifa lenye miundombinu ya TEHAMA na wafanyakazi na jamii inayoweza kutumia TEHAMA ina fursa ya kuzalisha bidhaa na huduma kwa ufanisi wa juu, kuongeza tija na kukuza uchumi.
Nguzo ya kumi ni ukubwa wa soko. Ukubwa wa soko unatoa fursa kwa uzalishaji mkubwa unaopunguza wastani wa gharama za uzalishaji. Nchi zenye soko kubwa la ndani inaweza kuanzisha na kuimarisha kampuni za uzalishaji kwa kutegemea soko la ndani. Katika ulimwengu wa utandawazi, soko la dunia linatoa fursa kwa nchi ndogo, kupunguza wastani wa gharama za uzalishaji kwa kuuza bidhaa na huduma zake kwenye soko la nje ya nchi. Kwa nchi ndogo kushiriki katika soko la dunia hasa kwa kuuza bidhaa za viwandani kunaongeza kasi ya kukua kwa uchumi.
Nguzo ya 11 ni kuwepo kwa kampuni na ufanyaji biashara wa kisasa. Kampuni ndio vituo vya uzalishaji vinavyotumia teknolojia mpya kuongeza ufanisi na tija. Ubora wa mtandao wa biashara na kuwepo kwa kampuni za kisasa zenye mikakati na uendeshaji wenye ufanisi kunaongeza tija na kuchochea ukuaji wa uchumi. Nguzo hii ni muhimu zaidi kwa nchi zilizo mstari wa mbele katika maendeleo ya uchumi. Klasta (kishada) za kampuni za kisasa katika eneo moja zinasaidia sana katika uvumbuzi wa teknolojia mpya za uzalishaji wa bidhaa na usambazaji wa huduma. Klasta ya bonde la silicon (Silicon Valley), California, Marekani limechangia katika uvumbuzi mbalimbali wa TEHAMA.
Nguzo ya 12 ni uwezo wa uvumbuzi wa teknolojia mpya za uzalishaji wa bidhaa na usambazaji wa huduma. Uvumbuzi wa teknolojia mpya ndiyo unaochochea ukuaji na maendeleo ya uchumi kwa nchi zilizoko mstari wa mbele wa maendeleo kama vile Marekani, Ujerumani, Japan, Uswidi (Sweden) Uingereza, Uswissi (Switzerland) na zinginezo.
Nguzo hizi 12 za ushindani wa kiuchumi wa kimataifa zinahusiana. Nchi ikiwa dhaifu katika eneo moja basi kutakuwa na uwezekano wa kuwa dhaifu katika maeneo mengine. Kwa mfano uwezo wa uvumbuzi wa teknolojia hauwezi kuwepo bila kuwa na raslimali watu yenye afya njema na elimu nzuri na yenye uwezo wa kumudu teknolojia. Mfumo mzuri wa benki na soko la mitaji unahitajika ili kuhakikisha uvumbuzi wa teknolojia mpya yenye tija unafikishwa sokoni na kutumiwa katika uzalishaji wa bidhaa na usambazaji wa huduma.
Umuhimu wa nguzo moja moja kati ya nguzo zote 12 katika kuongeza ushindani wa kiuchumi wa mataifa na kwa hiyo kuchochea ukuaji wa uchumi unategemea hatua ya maendeleo iliyofikiwa na nchi husika. Njia bora ya Tanzania kuongeza ushindani wake wa kiuchumi siyo sawa na Uswidi kwani Tanzania ni maskini ina miundombinu mibovu na Uswidi iko mstari wa mbele katika maendeleo ya kiuchumi na teknolojia. Mishahara ya Uswidi ni ya juu wakati mishahara ya Tanzania ni ya chini na wananchi wachache sana wenye ajira za uhakika. Watanzania wengi wanategemea kilimo cha kujikimu na sekta isiyo rasmi.
Ukuaji wa uchumi katika nchi ambazo ziko chini kimaendeleo kama vile Tanzania kunategemea utumiaji wa ardhi na maliasili nyingine, na nguvukazi isiyokuwa na elimu na mafunzo ya kutosha. Kampuni zake zinashindana zaidi kwa bei za bidhaa za kawaida. Katika nchi zilizo katika hatua ya mwanzo ya maendeleo, ushindani wa kiuchumi unategemea nguzo ya kwanza ya asasi za uchumi, utawala na sheria, nguzo ya pili ya miundombinu, nguzo ya tatu ya utengamavu wa uchumi mpana (macroeconomic stability) na nguzo ya nne ya afya na elimu bora ya msingi.
Kwa kadri nchi inavyoendelea na kukamilisha matakwa ya nguzo ya kwanza mpaka ya nne ndivyo mishahara inavyoongezeka , ukuaji wa uchumi utategemea sana ongezeko la ufanisi katika uzalishaji na kuongeza ubora wa bidhaa. Katika hatua hii ya maendeleo iliyofikiwa na nchi kama Mauritius, Namibia na Afrika ya Kusini, ongezeko la tija na ukuaji wa uchumi unategemea nguzo ya tano ya elimu na mafunzo ya juu, nguzo ya sita ya ufanisi wa soko la bidhaa, nguzo ya saba ya ufanisi wa soko la ajira, nguzo ya nane ya maendeleo ya soko la mitaji na huduma za fedha, nguzo ya tisa ya utayari wa kiteknolojia, na  nguzo ya kumi ya ukubwa wa soko la ndani na uwezo wa kushindana katika soko la nje
Nchi zilizo mstari wa mbele katika maendeleo zinategemea zaidi nguzo ya 11 ya kuwepo kwa kampuni bora na ufanyaji biashara wa kisasa na nguzo ya 12 ya  uvumbuzi wa teknolojia mpya ili kuongeza ushindani wa kiuchumi. Lakini nguzo nyingine pia ni muhimu. Kwa mfano miundombinu ya Marekani ikiwa ni pamoja na barabara na reli zinahitaji ukarabati mkubwa. Vilevile ubora wa elimu ya msingi na sekondari wa Marekani hasa katika shule za serikali katika maeneo ya watu masikini umeporomoka sana na unahitaji sera mwafaka ili ubora wa shule hizi ukaribie shule za nchi nyingine zilizoendelea.
Katika Taarifa ya WEF ya mwaka 2012/13, Rwanda imepanda nafasi 7  na kuwa ya 63 ukilinganisha na Taarifa ya mwaka 2011/12 ambapo ilikuwa ya 70. Rwanda inasifika kwa kuwa na asasi imara zinazozuia rushwa. Soko la ajira lina ufanisi na mnyumbuliko wa kutosha. Mabenki na soko la mitaji yameimarika na yanafanya kazi nzuri ya kukusanya akiba na kuwekeza vitega uchumi. Rwanda imewekeza kwenye TEHAMA na kuongeza kwa kiasi kikubwa utayari wake wa kiteknolojia. Kwa kuwa Rwanda haina bandari, ushindani wake wa kiuchumi unakwazwa na miundombinu ya nchi jirani ambako inalazimika kupitisha bidhaa zake.
Tanzania ilikuwa ya 120 katika Taarifa ya WEF ya mwaka 2011/12 na bado imebakia katika nafasi hiyo katika Ripoti ya 2012/13. Tanzania iko chini sana katika ushindani wa kiuchumi kwa sababu ya miundombinu mibovu. Tanzania ni ya 132 kati ya nchi 144 kwa ubora wa miundombinu. Tanzania bado iko chini katika elimu ya sekondari na elimu ya juu. Inashikilia nafasi ya 137 kati ya nchi 144. Tanzania pia iko chini sana katika utayari wa kupokea, kumudu na kutumia teknolojia na hasa matumizi ya mtandao wa internet ambapo inashikilia nafasi ya 122.
Ili Tanzania iweze kushindana na kunufaika katika ulimwengu wa utandawazi inahitaji iwekeze katika miundombinu ya barabara, reli, bandari, viwanja vya ndege, ufuaji na usambazaji wa umeme, miundombinu ya maji safi na maji taka TEHAMA na kuboresha elimu ya msingi, sekondari na vyuo vikuu. Ikiwa Rwanda imeweza kuongeza ushindani wake wa kiuchumi hakuna sababu kwa nini Tanzania ishindwe kufanya hivyo. Nchi inahitaji uongozi wenye dira, uadilifu na matumizi mazuri ya fedha za umma kuimarisha miundombinu na kuwekeza kwenye elimu bora ya vijana. Bila kuimarisha ushindani wa kiuchumi hatuwezi kuongeza ajira katika sekta za uchumi za kisasa.