Friday, August 17, 2012

KAULI YA NAPE DHIDI YA CHADEMA NI KAMA MTU ANAEOGOPA KIVULI CHAKE

Mh Abdul Kambaya-
Naibu Mkurugenzi wa Habari,
Mahusiano na Haki za Binadamu
wa Chama cha Wananchi (CUF)
CUF –Chama cha Wananchi kimeshangazwa na Kauli ya Katibu Muenezi wa CCM, alietoa kwa Vyombo vya Habari na kukituhumu chama cha CHADEMA , kwamba kimeingia mikataba ya kufisadi na Wafadhili walionje ya Nchi kwa lengo la kutaka kuja kupora Mali ya Asili inayoendelea kugunduliwa hapa Nchini kwetu Tanzania. Katika maelezo yake Katibu huyo iliita kile kilichofanywa na CHADEMA katika HARAMBEE ya kutafuta Fedha ni USANII, na kwamba CHADEMA wanataka kuhalalisha mabilioni waliopata toka kwa Wafadhili wao, na kwamba CCM inaushahidi na inawafahamu Wafadhili hao.
CUF –Chama cha Wananchi kinashangazwa na kauli hii ya kisanii iliotolewa na CCM kupitia Katibu wake Muenezi, CCM ni Chama kinachoongoza Nchi, jambo ambalo walipaswa kusema sio kuishitaki CHADEMA kwa Wananchi bali ni kuzuia hayo babilioni na kuwataja hao wafadhili ambao wameingia Mikataba na CHDEMA kwa lengo la kuja kupora utajiri mkubwa unaoendelea kugunduliwa katika masiku ya hivi karibuni. CUF- Chama cha Wananchi kinaamini kwamba CCM na CHADEMA ni watoto wa familia moja , na Wanafadhili wanao wafadhili ni wa aina moja wa ndani na nje ya Nchi. Iwapo Chadema wameingia mikataba ya kupewa mabilioni ili baadae wataposhika Madaraka waweze kulipa mabilioni hayo kwa kutukmia Mali ya asili tulionayo, basi watakuwa wanaendeleza utaratibu ule ule wa CCM wa kuiuza Nchi kwa bei poa ili mradi wao wawepo madarakani kama ambavyo CCM inafanya hivi sasa kuingia Mikatba mibovu isiokuwa na Manufa na Wananchi ili mradi wao wawafurahishe Wafadhili wao.
CUF- Chama cha Wananchi kinaamini kwamba Mti wa Matatizo ya Nchi yetu, ni Mufumo mbovu unaoendesha Serikali yetu na Nchi kwa ujumla wake. Kuwa na Vyama vyenye tamaa ya Madaraka, kama CCM na Chadema, ni matokeo ya awali ya Mfumo mbovu wa Nchi yetu, na kukithiri kwa wizi na matumizi mabaya ya Fedha za Umma na ukiukwaji wa Haki za binaadamu ni matokeo ya kati ya Mfumo mbovu. Watanzania waliowengi kuwa masikini wa kutupwa, ukosefu wa huduma bora kwa jamii,kudumaa kwa maendeleo ya Nchi na ukosefu wa ajira ni Matokeo ya muda mrefu yanayosababishwa na Mfumo mbovu wa Nchi yetu. Kwa maana hiyo basi, CUF –Chama cha Wananchi kinaamini kwamba , njia sahihi ya kulinda Rasilimali zilizopo na zinazoendelea kugunduliwa ndani ya Nchi yetu, ni kuwa na Serikali ya Umoja wa Kitafa, Serikali ambayo itashirikisha Vyama vyote venye wabunge, na kwa utaratibu huo, kutakuwa hakuna Chama kitakachokuwa na maauzi ya pekee katika matumizi ya Rasilimali na Mali ya asili ya Nchi yetu. Jambo hili limekuwa linahubiriwa sana na CUF , lakini pia limekuwa linapingwa sana na CCM na Chadema na kwa mantiki hiyo,
CUF – Chama cha Wananchi hakioni tafauti ya CCM na Chadema kisera na kimtazamo. CUF kinawataka Watanzania waelewe kwamba, kinachonekana hapa ni kwamba ,Chadema inaonyesha imewazidi kete CCM huko kwa Wafadhili wa nje kama ilivyowazidi kete kwa ufadhili wa Sabodo ndio maana unaona CCM inapiga kelele.
CUF – Chama cha Wananchi kina wataka CCM waache kuogopa kivuli chao na badala yake washughulike na kubadili Mufumo unaoendesha Nchi yetu iwapo kweli wanataka mabadiliko ya Kiuchumi na Kijamii .

No comments:

Post a Comment